Zaburi 130
Kuomba Msaada 
 
Wimbo wa kwenda juu. 
 
1 Kutoka vilindini ninakulilia, Ee Bwana.   
2 Ee Bwana, sikia sauti yangu.  
Masikio yako na yawe masikivu  
kwa kilio changu unihurumie.   
   
 
3 Kama wewe, Ee Bwana, ungeweka kumbukumbu ya dhambi,  
Ee Bwana, ni nani angeliweza kusimama?   
4 Lakini kwako kuna msamaha,  
kwa hiyo wewe unaogopwa.   
   
 
5 Namngojea Bwana, nafsi yangu inangojea,  
katika neno lake naweka tumaini langu.   
6 Nafsi yangu inamngojea Bwana  
kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi,  
naam, kuliko walinzi  
waingojeavyo asubuhi.   
   
 
7 Ee Israeli, mtumaini Bwana,  
maana kwa Bwana kuna upendo usiokoma,  
na kwake kuna ukombozi kamili.   
8 Yeye mwenyewe ataikomboa Israeli  
kutoka dhambi zao zote.