Zaburi 15
Kitu Mungu Anachotaka 
 
Zaburi ya Daudi. 
 
1 Bwana, ni nani awezaye kukaa  
katika Hekalu lako?  
Nani awezaye kuishi  
katika mlima wako mtakatifu?   
   
 
2 Ni yule aendaye pasipo mawaa,  
atendaye yaliyo haki,  
asemaye kweli toka moyoni mwake,   
3 na hana masingizio ulimini mwake,  
asiyemtenda jirani yake vibaya,  
na asiyemsingizia mwenzake,   
4 ambaye humdharau mtu mbaya,  
lakini huwaheshimu wale wamwogopao Bwana,  
yule atunzaye kiapo chake  
hata kama anaumia.   
5 Yeye akopeshaye fedha yake bila riba,  
na hapokei rushwa dhidi ya mtu asiye na hatia.  
   
 
Mtu afanyaye haya  
kamwe hatatikisika.